KAULI ZA NASAHA KATIKA HARUSI ZINAVYOJENGA UHUSIANO WA WANANDOA:

No Thumbnail Available
Date
2021-12-01
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
SUZA
Abstract
Utafiti huu ulikuwa na lengo la kuchunguza kauli za nasaha katika harusi za Wapemba jinsi zinavyojenga uhusiano wa wanandoa. Utafiti ulikuwa na malengo mawili: Kuainisha kauli za nasaha anazopewa biharusi na bwanaharusi kwa mujibu wa utamaduni wa jamii ya Wapemba na kufafanua uhusiano wa ndoa unaojengwa na kauli hizo. Utafiti uliongozwa na nadharia ya uchambuzi makini wa matini. Utafiti ulifanyika katika wilaya mbili, Chake chake na Mkoani. Data zilikusanywa kupitia mbinu ya dodoso, usaili na ushuhudiaji. Sampuli ya watafitiwa thelathini (30) ilitumika. Utafiti umebaini kuwa kauli za nasaha zitolewazo katika harusi za Wapemba. Ziko kauli za nasaha ambazo zimefanana na zinajenga uhusiano baina ya biharusi na bwanaharusi katika maisha ya ndoa. Mfano “Jihadhari sana, usimruhusu mke kuwa na marafiki wengi na kutumia muda mwingi nje kwa kukaa na marafiki zake.” “Tahadhari sana na ulimi, tunakunasihi, ulimi wako unatakiwa utumie vizuri.” Pia mtafiti amegundua kauli za nasaha zimefanikiwa kuonesha uhusiano unaojengwa na kauli hizo kwa bwanaharusi na biharusi. Mfano wa kauli za nasaha zinazojenga uhusiano kwa bwanaharusi na biharusi: “Tunakunasihi, mke ni mkeo, ndio mwenzio usimfanyie jeuri wala dharau.” “Zingatia vizuri tunayokunasihi, umuheshimu mumeo umuone ni mumeo wala simdharau.” Mtafiti anapendekeza kuwa kauli za nasaha ziendelee kutumika katika jamii ya Wapemba na jamii nyengine za Waswahili. Pia mtafiti anapendekeza uchunguzi zaidi ufanyike katika uwanja wa kitaaluma utakaohusisha kauli za nasaha katika miktadha tafauti ikiwemo msibani, maofisini, mashuleni na miktadha mengineo ili kuzijenga jamii kuwa na maadili bora katika sehemu zote napokuwepo. Pia mtafiti anapendekeza watafiti wengine waangalie kauli za nasaha walizopewa wanandoa wakongwe na wanandoa wa sasa halafu walinganishe wepi waliofanikiwa kudumu katika ndoa zao.
Description
Utafiti uliongozwa na nadharia ya uchambuzi makini wa matini. Utafiti ulifanyika katika wilaya mbili, Chake chake na Mkoani. Data zilikusanywa kupitia mbinu ya dodoso, usaili na ushuhudiaji. ampuli ya watafitiwa thelathini (30) ilitumika. Utafiti umebaini kuwa kauli za nasaha zitolewazo katika harusi za Wapemba. Ziko kauli za nasaha ambazo zimefanana na zinajenga uhusiano baina ya biharusi na bwanaharusi katika maisha ya ndoa. Mfano “Jihadhari sana, usimruhusu mke kuwa na marafiki wengi na kutumia muda mwingi nje kwa kukaa na marafiki zake.” “Tahadhari sana na ulimi, tunakunasihi, ulimi wako unatakiwa utumie vizuri.”
Keywords
Citation