• Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  • Researches
  • SUZA Repository
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Mohammed Ali, Msellem"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Tathmini ya Mazingira ya Kijamii katika Kujifunza Kusoma Kiswahili kwa Watoto wa Kigeni Zanzibar
    (SUZA, 2019-12-01) Mohammed Ali, Msellem
    Utafiti huu umetathmini Mazingira ya Kijamii katika kujifunza kusoma kwa watoto wa kigeni wanaojifunza Kiswahili kama lugha ya kigeni Zanzibar. Jumla ya watoa taarifa 28 walishiriki katika utafiti huu waliogawanyika katika makundi mawili: wajifunzaji lugha 16 na wazazi/walezi wao 12. Utafiti ulifanyika katika skuli ya Kimataifa ya Feza iliyopo Mjini Magharib Zanzibar na katika kaya za wazazi/walezi wa wajifunzaji lugha ya Kiswahili zilizopo Mjini Magharib. Katika kukusanya data, utafiti umetumia kipimo cha kusoma ili kubaini uwezo walionao watoto wa kigeni katika kusoma matini za Kiswahili pamoja na mbinu ya usaili kubaini dhima ya Mazingira ya Kijamii. Aidha, utafiti ulitumia hojaji za kuchunguza mambo ya Mazingira ya Kijamii wa watoto wa kigeni. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Ukuzaji Stadi ya Kusoma ya Clay (1966) na Holdaway (1979). Hoja kuu ya nadharia hii ni mchangamano wa kimazungumzo na kusoma pamoja baina ya anayejifunza kusoma na wajuzi wa lugha husika. Vilevile, mchangamano baina ya mjifunzaji kusoma na vitabu vya lugha lengwa ni miongoni mwa misingi mikuu ya ujifunzaji kusoma kwa mujibu wa Nadharia ya Ukuzaji Stadi ya Kusoma. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba dhima ya Mazingira ya Kijamii katika kujifunza kusoma Kiswahili kwa watoto wa kigeni ni kuwawezesha watoto kupata kuchanganyika na marafiki wanaojua Kiswahili wakiwa katika Mazingira ya Kijamii. Aidha, kuchanganyika na wazazi/walezi wanaotumia Kiswahili pamoja na tabia binafsi ya watoto kujisomea maandiko ya Kiswahili wakiwa katika Mazingira ya Kijamii pia vimechangia uwezo wa kusoma walionao watoto wa kigeni. Vilevile, imependekezwa kwa watafiti wengine kufanyika utafiti kuhusu ufundishaji na ujifunzaji wa stadi nyengine za lugha ya Kiswahili katika Mazingira ya nje na ndani ya darasa.

Contacts

  • Director of library Service.
  • P.O BOX 146, Zanzibar
  • library@suza.ac.tz
  • suza.ac.tz
  • Main Campus.
  • Tunguu, Zanzibar, Tanzania

Other Resources

  • Open Access Policy
  • Open Data
  • Term of Use
  • Frequently asked questions (FAQ)

The State University of Zanzibar. © 2025.

  • Cookie settings
  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback