• Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  • Researches
  • SUZA Repository
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "ALAWY, Zaharia Mohamed"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Taathira za Ubabedume kwa Mwanamme Mwenza wa Kizanzibari Kupitia Nyimbo za Taarab Asilia
    (The State University of Zanzibar (SUZA), 2018-12) ALAWY, Zaharia Mohamed
    Tasnifu hii imelenga kuchunguza taathira za ubabedume kwa mwanamme mwenza wa Kizanzibari kupitia nyimbo za taarab asilia. Data zilikusanywa, zilichanganuliwa na matokeo yakabainishwa. Sura ya kwanza imebainisha usuli wa mada na tatizo la utafiti, ambalo ni uwelewa mdogo wa jamii kuhusu taathira za ubabedume kwa mwanamme mwenza katika jamii ya Wazanzibari. Utafiti uliongozwa na lengo kuu na malengo mahsusi. Sura ya pili ilizungumzia kazi tangulizi, mapitio kuhusiana na ubabedume, nyimbo na mapitio ya nyimbo za taarab. Aidha, ilizungumzia Nadharia ya mwitiko wa Msomaji na Nadharia ya Semiotiki. Sura ya tatu, ilionesha mbinu ya mahojiano iliyotumika kukusanyia data na hatua za mchanganuo wake. Mbinu ya maelezo ilitumika katika kuchanganua data na kupewa vifupisho. Sura ya nne imebainisha ubabedume ulivyojitokeza, uchambuzi wa taathira zake na hatua za kupambana na taathira hizo. Sura ya tano imeeleza kwa ufupi matokeo ya utafiti ambayo yamejitokeza kwa namna mbili, nyimbo zenye ubabedume wa wazi na zenye ubabedume uliojificha. Ndani yake mmejitokeza ubabedume wa kejeli, masikitiko, kuumiza moyo, malumbano na kutahadharisha. Pia taathira za woga, visasi, maradhi, msongo wa mawazo na kuhalalisha maovu. Utafiti umependekeza hatua za kuchukuwa kupunguza kasi ya ubabedume kwa mwanamme mwenza, kupewa taaluma kwa kutumia vyombo vya habari, kuwekea vitengo vya kushughulikiwa matatizo yao. Kazi hii imechangia kuongeza taaluma ya ubabedume kwa mwanamme katika jamii ya Wazanzibari. Hitimisho na mapendekezo ya utafiti uliofanyika yameoneshwa kwa ajili ya tafiti zijazo.

Contacts

  • Director of library Service.
  • P.O BOX 146, Zanzibar
  • library@suza.ac.tz
  • suza.ac.tz
  • Main Campus.
  • Tunguu, Zanzibar, Tanzania

Other Resources

  • Open Access Policy
  • Open Data
  • Term of Use
  • Frequently asked questions (FAQ)

The State University of Zanzibar. © 2025.

  • Cookie settings
  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback